BONGO MOVIE MSIKILIZENI RAY



 Na Melkiory Gowelle



Wasanii wa filamu nchini, wametakiwa kupambana katika kutengeneza kazi zenye viwango ili kuwarudisha Watanzania katika soko lenye ubora wa hali ya juu kama ilivyokuwa hapo awali.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es salaam na msanii mkongwe wa tasnia hiyo bongo, Vicent Kigosi ‘Ray’  katika kipindi cha Jahazi kinacho rushwa na Clouds fm.

Ray amesema kuwepo kwa utitiri wa filamu za kibongo zilizokosa ubora katika soko, kumesababisha kupanda kwa thamani ya filamu za kigeni zikiwemo za kizungu na zakikorea.

“Unajuwa sehemu yeyote yenye biashara basi kila mtu anataka kuingia ili afanye biashara bila kuzingatia viwango na ubora wa biashara hiyo. ” alisema Ray.

“Sasa hivi Watanzania wameamka, kwahiyo tengeneza kitu kizuri watu watakichukuwa tu, sawasawa na kupika chakula kizuri  ambacho watu lazima wale.” Aliongeza Ray.

Ray amepania kurudisha hadhi ya filamu za Kitanzania kupitia filamu yake mpya iitwayo 'GET KIPPER' inayo tarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.
Share on Google Plus

About BASEMENT255

0 comments:

Post a Comment