WANANCHI WATEKELEZA AGIZO LA KUACHA KUTUMIA POMBE AINA YA VIROBA.


                                                   

                                                                     
Na, saphinia seleman.
  Baada ya Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Majaliwa kassimu Majaliwa kupiga marufuku pombe aina ya viroba, wananchi wameanza kutekeleza agizo hilo.

     Mh, Majaliwa alitangaza rasmi ifikapo tarehe 1 mwezi wa tatu 2017 pombe hiyo isionekane mitaani na yeyote atakaebainika kutumia kilevi hicho atapigwa faini ya shilingi elfu 50000.

        Tamko hilo limeleta mtazamo chanya kwa wananchi wa mtaa wa mbezi beach "A "makazi mapya ambapo  wamekubaliana na agizo la Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

         Akizungumza na mwandishi wa habari mjumbe wa mtaa huo bi, Mwajuma Mnamba amesema atafuatilia kuhakikisha kila mmoja anazingatia agizo hilo. 


Share on Google Plus

About BASEMENT255

0 comments:

Post a Comment