KUNA MENGI NYUMA YA MAREFA WETU JAMANI!!!!!
           NA  TAGATO JAMES TAGATO   



                  Mwamuzi katika mchezo wa mpira wa miguu ananafasi kubwa, lakini pia ni kiungo muhimu katika kuhakikisha  anatafsiri vizuri sheria 17 za mpira uwanjani.Mwamuzi huyu pia ni binadamu ndio manaa huwa anakuwa na wasaidizi ili kuhakikisha anapunguza mapungufu yake pindi awapo uwanjani.
                  Nchini kwetu Tanzania waamuzi wameonekana ni moja kati ya kikwazo sugu kinacho kwamisha maendeleo ya soka letu,huku pia wakizibeba lawama nyingi sana za mashabiki pamoja wa wadau wengi wa masuala ya mpira nchini.
                Lakini kinacho nishangaza ni kwanamna gani tunawapa lawama watendaji wakati hatujui  ni mfumo upi unamfanya mwamuzi kuwa na vigezo vya kuchezesgha ligi kuu?
                Ngoja nkupe mfano wa soka la nchi ya Uingereza wao mpaka mwamuzi afikie kuchezesha ligi kuu lazima apitie tena kwa performance ya hali ya juu kwenye level zi sizo pungua kumi na moja tena kulinga na umri.
                 Lakini nchini kwetu ni rahisi mno,yani kozi ya wiki mbili mazoezi kwa vitendo utachezesha daraja la tatu na la nne, kisha unakwenda tena kozi una pandishwa hadi juu daraja la pili,la kwanza na hatimaye ligi kuu.Sasa ukiutazama huu mfumo unaweza kuona ni namna gani marefa wetu wanapitia njia raihisi kuchezesha michezo migumu.
             Mbali na mfumo lipo suala kubwa la maslahi,kiukweli hapa ndio soka letu limeoza kabisaa.Kiukweli waamuzi hawa huishi katika mazingira magumu ya vishawishi vya timu zetu ziinazo jiita kongwe.Hapa ndipo mwamuzi anapo jikuta anachukua jukumu la kubeba lawama ilimradi maisha yake yasonge tu mana pesa wanayoipata haikidhi mahitaji yao kiukweli.
             Hapa litakataliwa goli hapa utanyimwa penalty hapa utapewa umeme (yaani kadi nyekundu) mala vile basi vulugu tupu lakini mwisho wa siku yeye anatoa maamuzi yake kumbeba aliye weka mzigo mezani.
                   Lakini jingine na lenye mantiki kubwa ni ukweli utabakia pale pale kuwa kama unajiendesha bila mtu wa kukuangalia nini na wapi unakosea, basi we utakuwa wa kukosea kila siku mana unajua hakuna wa kukuliza.Lakini pale England wao wana jopo la waamuzi na kimsingi hili hu shughurikia maswala mengi yanao wahusu waamuzi lakini jopo hili huwa ndani ya FA
                   Kama unakumbuka sakata la mwamuzi Mike Dean kushushwa hadi ligi daraja la kwanza badaa ya kuvurunda kweny michezo kama Liverpool alipiocheza na Everton lakini pia akatoa kadi nyekundu isiyo halali kwa Soufiane Feghuli wa kati Westham ilipo ikabili Manchester United.

Kwa wenzetu ni rahisi kutoa maamuzi haya baada ya kupita mikanda ya mchezo husika lakini pia ripoti ya mwamuzi.Sasa huku kwetu kwanza ripoti itafika sawa lakini je atawajibishwa?ngoja tusubiri ile ya juzi si wote tuliiona lakini ile itapigwa chini kimya kimya mi yangu Macho tu.
Share on Google Plus

About BASEMENT255

0 comments:

Post a Comment