NAPE AMVULIA KOFIA DITTO



Na. Melkiory Gowelle 


Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Mosses Nnauye amempongeza msanii wa bongo fravour Ditto Lameck ‘Ditto’ kwa ubunifu wa mashairi makali ya wimbo wa Moyo sukuma damu.


Akizungumza Jijini Dar es salaam Nape amesema sio jambo rahisi katika muziki kufikiria kitu tofauti na wengine na kutumia ubunifu wa kukiwasilisha katika jamii.


“Ni tatizo lipo katika jamii, jambo lipo katika jamii, lakini namna unavyo liwasilisha unatumia sanaa fulani, utaalam Fulani na ubunifu ambao unagusa akili za watu mpaka wakakubali kuwa kazi ya moyo ni kusukuma damu, hivyo ukichanganya na mambo mengine unasababisha matatizo.” Amesema Nape. 


Share on Google Plus

About BASEMENT255

0 comments:

Post a Comment