HAZARD AMWAGIA SIFA CANTE


Na Tagato James Tagato


Mshambuliaji mwenye asili ya Ubeligiji na klabu ya Chelsea fc Eden Hazard amemmwagia sifa mchezaji mwenzie N’golo Cante akimtaja kama ni moja kati ya viungo bora.kauli hiyo ameitoa alipokuwaz akihojiwa baada ya mchezo uliowakutanisha na Westham na ukamalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi wa goli 2-1.





Hazard alisema “yeye(Cante)ni moja kati ya viungo bora na wakati mwingine huwa najihisi nacheza na pacha wangu uwanjani nikiwa nae”
Sifa hizi zimekuja baada ya Cante kutoa mchango mkubwa kwenye goli la kwanza lililofungwa na Eden Hazard katika dakika ya 25 ya mchezo huku pia akiwa muhimili  muhimu katika safu ya ulinzi wa timu hiyo.



Alipo ulizwa kuhusiana na mchezo huo Hazard alisema “hakika hatukucheza mchezo mzuri lakini tulijilinda vizuri na tulistahili ushindi”

Sasa Chelsea anakaa kileleni mwa msimamo wa EPL (English premier league)kwa tofauti ya alama 10 huku ikiwa imesalia michezo 12 pekee ili ligi hiyo ifikie tamati



Share on Google Plus

About BASEMENT255

0 comments:

Post a Comment